https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, October 25, 2013

Mapacha Watatu kusherehekea miaka minne


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya Mapacha Watatu, inatarajia kufanya sherehe ya kutimiza miaka minne tangu kuanzishwa kwake Ijumaa ya Novemba 15 katika Ukumbi wa Letasi lounge, zamani Business Park, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Mapacha Watatu, Jose Mara pichani.
Onyesho hilo la kihistoria limepangwa kufanyika kwa ajili ya kuwashukuru wadau na mashabiki wao kutokana na kuwaunga mkono kwa miaka kadhaa sasa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa bendi hiyo, Khamis Dacota, alisema kuwa mipango ya kuhakikisha kuwa bendi yao inafanya sherehe ya miaka minne inaendelea.

Alisema lengo lao ni kuwashukuru mashabiki wao kwa kuimba vibao motomoto vyenye kukonga nyoyo za wapenzi wao, hivyo ni jukumu la wadau hao kuingia kwa wingi kwenye shoo hiyo.

“Tumefanya mpango wa kufanya sherehe hii ya kutimiza miaka minne katika ukumbi wa Letesi, huku tukiamini ndio eneo murua kwa ajili ya kuwashukuru mashabiki wetu.

“Litakuwa ni onyesho la aina yake, ukizingatia kuwa Mapacha Watatu ni bendi imara yenye kila sababu ya kufanya vizuri katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini,” alisema.

Mapacha Watatu ipo chini ya Khalid Chokoraa na Jose Mara, huku muasisi mwingine wa bendi hiyo Kalala Junior akiamua kurudi katika bendi yake ya zamani The African Stars, Twanga Pepeta.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...