https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, October 31, 2013

Ukumbi wa mazoezi ya ngumi za ridhaa Tanga kikwazo kwa mchezo huo


Na Oscar Assenga,Tanga.
CHAMA cha Ngumi za Ridhaa mkoa wa Tanga(TBA)kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutokuwa na ukumbi wa kufanya mazoezi kwa mabondia kitendo ambacho kinawapa wakati mgumu mabondia wakati wa kufanya mazoezi. 



Mwenyekiti wa Chama hicho,Mansour Soud Semfyoa aliiambia Tanga Raha kuwa hali hiyo inawafanya mabondia hao kushindwa kutimiza ndoto zao na kuziomba mamlaka husika ikiwemo uongozi wa serikali ya wilaya kuwasaidia ili kuweza kupatikana ukumbi wa mazoezi.

Soud alisema suala lengine ambalo linawapa changamoto ni uhaba wa vifaa vya kufanyia mazoezi kwa mabondia waliopo mkoani hapa hivyo kuwaomba wadau kuwasaidia ili viweze kupatikana.
Mwenyekiti wa Chama Cha Ngumi za Ridhaa mkoani Tanga, Mansour Soud Semfoya
Mwenyekiti huyo alisema chama hicho kimefanya jitihada mbalimbali ili kuweza kupatikana ukumbi wa Tangamano ambapo uongozi wa chama hicho  tayari umeshaandika barua kwenda kwa mkurugenzi wa Jiji lengo likiwa ni kumuomba wautumia ukumbi wa Tangamano.

Alisema majibu ya barua hiyo iliwajibu wamekubaliwa katika ukumbi wa Communite Centre Makorora ambapo wataungana na vikundi vyengine na kuelezwa kuwa wanatakiwa walipie sh.elfu hamsini ili waweze kupewa eneo hilo.

Aidha alisema mikakati waliokuwa nayo hivi sasa ni kuuendeleza mchezo wa ngumi ambao unaonekana kupotea mkoani hapa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali lengo likiwa ni kupata mabondia wazuri ambao watautangaza mkoa huu.

Aliongeza kuwa wanampango wa kuupeleka mchezo huo mashuleni ambapo kwa kuanzia wataanzia katika shule za msingi na sekondari na baadae vyuo vikuu lengo ni kuwapa vijana hao uelewa kuhusu mchezo huo.

Soud alisema pia wanatarajia kuanzisha miradi ambayo itakisaidia chama hicho kujiendesha chenyewe kuliko kutegemea misaada ambao wakati mwengine inaweza kukwamisha malengo yao waliojiwekea.    

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...