https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 29, 2012

Watanzania waaswa kupenda bidhaa za nyumbani



Mkurugenzi wa Grace Products, Elizabeth Kilili

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MJASIRIAMALI na Mkurugenzi wa Kampuni ya Grace Products Ltd, Elizabeth Kilili, amewataka Watanzania kupenda bidhaa za nyumbani ili kuziletea tija na hatimae zivuke mipaka.

Akizungumza na Handeni Kwetu jijini Dar ess Salaam leo asubuhi, Elizabeth alisema kwamba bila Watanzania wenyewe kupenda bidhaa za Kitanzania, haziwezi kufanikiwa.

Alisema biashara nyingi zinahitaji fedha, hivyo kama wapo walioamua kuwekeza humo na wateja wenyewe wakiangalia bidhaa za nje, wajasiriamali wa ndani hawawezi kuendelea.

"Tunaomba Watanzania wapende bidhaa zetu kama vile sabuni, mafuta, shampoo na nyingine zinazoandaliwa ndani yaa nchi na sio waangalie vitu kutoka nje ya nchi, ambavyo nyingine si nzuri.

"Tukifanya hivyo tutaweza kufanya vizuri katika soko la ndani na kuweka nguvu kuuza na nje ya nchi, ukizingatia kwamba fedha zinazoingia kwenye mzunguuko zinarudi kutokana na biashara kuungwa mkono,” alisema.

Mwanamama huyo ameingiza madukani bidhaa nne, ikiwamo sabuni ya kuogea ya Grace Manjano, mafuta ya kupaka, shampoo, sabuni ya kuoshea vyombo na chooni, ambazo zote hizo zina uwezo mkubwa wa kupambana na magonjwa ya ngozi na kukuacha mwili wa binadamu kuwa na afya nzuri na mvuto wa aina yake.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...