https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, December 31, 2012

Salamu za mwaka mpya za Dayna Nyange



Mambo vipi ndugu zangu? Napenda kuchukua nafasi hii kuwatakia maandalizi mema ya mwaka mpya. Mungu atupe nguvu na neema zaidi katika mwaka 2013 utakaoanza kesho. 

Mwaka 2012 tutaukumbuka kwa mengi yapo mema na mabaya. Naomba nikuombe radhi wewe kwa lolote ambalo niliwahi kukukosea, nawe kama ulinikosea sina tatizo nawe tangu sasa.

Pia naomba nitoe shukrani zangu kwa wote waliohusika ktk mafanikio yangu ya kimuziki. 

Dayna Nyange

Naamini wengi mlikuwa mstari wa mbele katika kunishauri, kunipongeza na kunikosoa nilipokosea. Shukrani nyingi zwafikie radio presenter, dj's, radio na tv zote Tanzania na Afrika, maana bila nyinyi kuzicheza nyimbo zangu nisingefika hapa.
Hapo vipiiii
 
Waandishi wa magaazeti mlikuwa mstari wa mbele katika kuona nafika mbali kwa kuandika habari zangu na kufika hata vjijini. Nachukua fursa hii kuwashukuru pia blogs mbalimbali.

Mlikuwa mstari wa mbele kwakuandika habari na ku-post hata baadhi ya show zangu ambazo mmenipa heshma ya kufika mbali zaidi na kusikika hata nje ya nchi mchango wenu ni mkubwa.
Pozi za Dayna Nyangeeeeee

Pia requester wa media sina cha kuwalipa nawashukuru sana na nitabaki kuwaheshimu kwani mmetoa mchango mkubwa kwa kuomba nyimbo zangu media na zikachezwa.

Na amini ni mchango mkubwa sana ktk game hasa kwetu wasanii Nitabaki kuwaheshimu na kuwathamini siku zote. Bila kuwasahau wasanii wenzangu walikuwa nami bega kwa bega katika kunishauri na kunisaidia kwa chochote.

Pia ma dj wa club mbalimbali, mmekuwa chachu ya mzk wangu pale mlipoonesha ushirikiann wenu kwangu.

Pia Waandaaji wa (show) matamasha  madogo na makubwa nawashukuru sana sana kwa kuniamini na kukubali kufanya kazi na mimi siwasahau ma-producers wa video na Audio  na studio mbalimbali kwa kunifanyia kazi za uhakika na jamii ikanikubali kwa kazi hizo.

Wote kwa pamoja naamini sasa ni kama ndugu. Nawaomba muonyeshe tena moyo huwo na mwaka ujao na mingine kwani kaz nzur ni yenye kushirikiana.

Msisite kama ntawakosea naomba msisite kunikanya na kunisamehe. Napenda wote na kuwajali. Nawatakia  mwaka mpya.

Its me Dayna Nyange ‘Mkali wao’

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...