https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, December 27, 2012

Mr Nice aliyewika na kutoweka Tanzania



Huyu ni Mr Nice, mkali aliyetokelezea sana kabla ya kutoweka katika 'game'
 
ALITOKELEZEA

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MWIMBAJI na mfalme wa muziki wa Takeu aliyousisi kwa Tanzania, Nice Lucas Mkenda maarufu kama Mr Nice ni miongoni mwa wasanii waliowahi kuvuma mno miaka ya nyuma. Kila mmoja alikuwa akipenda kumuona nyota huyo.

Nyimbo alizowahi kutoa msanii huyo ni pamoja na Mama, Kikulacho, Rafiki, Fagilia na nyinginezo ambazo hakika watu walizipenda na kuziheshimu.


Sio Tanzania tu, bali nchi nyingi za Afrika Mashariki na Kati, Nice alipendwa na kukubalika mno.

Nakumbuka, Nice ilibaki kidogo aonekane kama Rais, kwani nchini Msumbiji, visiwa vya Comoro, Uganda, Kenya, Rwanda jina lake lilivuma na wadau wengi walisema kumbi za kufanya shoo jamaa huyo zilikuwa chache, huku viwanja vya wazi ndio ilikuwa mahali pake.

Huyu Mr Nice alivuma balaa
 
Watoto mtaani walikuwa wakicheza au kunyoa kama Mr Nice, hasa ile style yake ya kunyoa unga unga na kupaka rangi nyeusi na kutelezesha mstari sehemu ya sikio na kuonekana nadhifu.

Kuvuka kwake kulizidi hasa alipokuwa akiingia kwenye ugomvi na kupigwa mara kwa mara na nyota mwenzake, Godfrey Tumaini, maarufu kama Dudu Baya, a.k.a Zeze Dudu.

Wengi walimlilia sana waliposikia anaonewa ovyo na Dudu Baya. Pamoja na sifa zote hizo, heshima yote hiyo, lakini hali ni mbaya. Jamaa huyo hasikiki tena jukwaani.

Imefikia wakati mwaka unakwisha bila kuonekana jukwaani. Katikati ya mwaka huu alionekana kwenye shoo ya Fiesta ya mjini Moshi, watu wakasema jamaa anataka kurudi tena?

Kwanini? Uwezo wake umeisha? Anaishi vipi? Wadau wa burudani tunakutana naye katika baadhi ya kumbi za starehe akipata moja moto moja baridi, hasa kwa wale wanaoendelea kumheshimu kumpa ofa.

Sasa basi, kama wewe ni swahiba wake, ndugu yake, Handeni Kwetu inataka kujua sanaa yake imeishaje? Mwambie kuwa tumemkumbuka sana. Mwambie aone nyota wapya wanavyovuna fedha kupita kiasi.

Hivi unajua kuwa kama leo hii Mr Nice angekuwa Diamond, Ommy Dimpozi sijui angeitwa nani. Majina yote yangekuwa yake, hasa yale Fremason kama wanavyozushiwa wengine.

Nakusalimia bwana Mr Nice kama kweli uwezo unao tukutane jukwaani kwa nyimbo nzuri na zitakazorudisha heshima yako, vinginevyo tutaendelea kusema kuliwahi kuwa na Mr Nice.

0712 053949
0753 806087

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...