https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, December 31, 2012

Tetea msimamo wako wa kimapenzi


Mapenzi matamu ehee?
 
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
HII ni Jumatatu ya mwisho kwa mwaka huu 2012 kabla ya kuipokea mwaka mpya utakaoingia siku nne zinazokuja.

Jumatatu hii inatufanya tuendelee kuwa pamoja katika kona ya uhusiano wa kimapenzi na kimaisha.

Nakushukuru kwa dhati kwa wewe uliyeijali na kuithaamini kona hii katika kipindi chote cha mwaka huu, huku nikiamini utaendelea kuniunga mkono.

Nitakuwa mchoyo wa fadhira kama nitashindwa kukushukuru wewe, maana unatumia muda wako mwingi kuisoma na kuamua kunipigia simu kwa ajili ya kuchangia yanayoandikwa humu kila mwisho wa wiki.

Ndugu msomaji wangu mpendwa, katika mapenzi hakuna kitu kizuri kama kuheshimu maamuzi ya moyo wako na pia kusimama kwenye msimamo wako. Nasema hivyo, maana wengineo wanayumba kwakukosa msimamo.

Wanajua fika kuwa wameamua kukaa sehemo moja, lakini kwa sababu hiyo wanajikuta wakisikiliza maneno ya watu, jambo linalomvuruga kichwa chake na kuamua kwa mikono yake kuvunja uhusiano wake, iwe ni wa ndoa au uchumba.

Hilo ndio jambo kubwa na baya mno. Bila kuwa na msimamo wako, kamwe huwezi kufurahia mapenzi yako, maana duniani hakuna aliyekuwa sawa.

Kila mtu ana mapungufu yake. Hata hivyo katika hilo, huwezi kusikiliza majirani wanasema nini.

Huwezi kusikiliza marafiki zako wanakwambia kitu gani. Ndio anaweza kuwa tofauti mpenzi wako kwa marafiki au ndugu zako, ila jua kabisa hupo kwa ajili ya watu hao wanaokwambia maneno ya kila aina yanayohusu mtu wako.

Wapo watu waliobarikiwa uongo. Ni hao wanaoweza kukwambia mtu uliyekuwa naye havutii kimuonekano wake, ila mwisho wa siku wewe mwenyewe ndio muamuzi wa jambo hilo, hivyo lazima uwe makini.

Ukiyumba wewe, hata uhusiano wako utayumba. Utaachana bure na mtu wako kwasababu ya hao wapita njia.

Ndio maana nasema lazima uwe na msimamo na uheshimu maamuzi ya moyo wako. Nasema hivyo, maana moyo hauwezi kudanganya.

Unapopenda hakuna mwingine anayeweza kutoa hoja ya aina yoyoye ikasikilizwa. Hapo lazima uwe makini.

Hapo lazima ujuwe ubaya wa mtu wako au uzuri wake wewe mwenyewe ndiyo unayejua, hivyo hakuna haja ya kujua watu wanasema nini.

Bila hivyo utayumba. Na mbaya zaidi tabia hiyo itaendelea kukusumbua katika maisha yako yote, kitu kitakachokufanya ubadilishe wapenzi au waume kila siku ya Mungu. Hawatakoma hao. Baaada ya kuachana na wako watahamia huko utakapokwenda.

Ndio kazi yao, maana hawapendi kukuona umetulia na kufurahia mapenzi kwasababu yako ya kuyumbishwa. Lazima ujitambuwe na kujifanyika marekebisho wewe mwenyewe.

Mapenzi ni matamu kweli, ila ni baada ya kujielewa na kuheshimu uhusiano wako. Ukiheshimu wewe mwenyewe na kusimama kwenye msimamo wako, hakuna mtu wa kukuletea habari za ajabu ajabu na ukazisikiliza.

Hata kama mtu huyo atakuja kwa nia ya kumponda mpenzi wako, mume wako au mke wako, unaweza kuwa mkali na kumkimbiza mtu huyo, endapo utabaini umedhalilishiwa mwendani wako, hali ya kuwa ndio chaguo lako.

Hakuna njia ya mkato katika hilo. Msimamo tu ndio kila kitu. Wapo marafiki ambao muda wao mwingi ni kuwaponda wapenzi wa wenzao na wenyewe wakacheka. Maana rafiki ni muhimu mno kwake kuliko mtu wake.

Huo ni ujinga. Ila kinachotakiwa hapo ni kuwa mkali, maana wanachotaka wao ni kuona uhusiano wako unakufa, hivyo lazima ujuwe.

Lakini ukiwa mkali kwa watu wenye tabia hizo, watakuogopa na kukuheshimu pia.

Huo ndio ukweli wa mambo. Na ukifanya hivyo, uhusiano wako, ndoa yako itadumu na kuwa kuwa yenye furaha wakati wote.

Jifanyie marekebisho msomaji wangu kwa faida ya uhusiano wako, maana mengi yasemwayo ukiyachekea utafadhaisha moyo wako.

0712 053949
0753 806087


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...