https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 29, 2012

Polisi-Mkutano wa Simba kesho marufuku



Kamanda wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela, akitangaza kuuzuia mkutano wa Simba uliopangwa kufanyika kesho, Travertine Hoteli, Magomeni.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni kwa kupitia Kamanda wake Charles Kenyela, limepiga marufuku mkutano wa Simba uliopangwa kufanyika kesho, Travertine Hoteli, Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage

Mkutano huo uliitishwa na wanachama wapatao 698 kwa ajili ya kujadili mambo yanayoihusu timu yao, ikiwa chini ya Mwenyekiti wao, Ismail Aden Rage.

Akizungumza muda mfupi uliopita, Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kamanda Kenyela alisema mkutano huo wa Simba sio halali kwakuwa haujaandaliwa kwa kufuata taratibu za kisheria.

Alisema wamepokea barua kutoka Makao Makuu ya Simba, na kusainiwa na Katibu Mkuu wao, Evodius Mutalawa wakiomba polisi wauzuie mkutano huo kwakuwa una lengo la kuleta vurugu na kuichanganya klabu yao.

“Huu mkutano sio halali maana hata jeshi la polisi halijapokea barua rasmi zaidi ya nakala inayoelezea kufika kwetu.

“Jeshi la polisi haliwezi kufanya kazi kwa nakala, hivyo naomba wote wajuwe kuwa hatuwezi kuruhusu mkutano huo na tunaomba Travertine wapinge wanachama hao kukutana kwenye hoteli yao,” alisema Kenyela.

Kuzuiwa kwa mkutano huo huenda ikawa karata nzuri kwa viongozi wa Simba waliowahi kutamka kuwa walioitisha mkutano huo ni wahuni, hivyo hawawezi kufanikiwa kuitisha mkutano huo.

Kwa wiki kadhaa sasa, wanachama hao wa Simba waliwakuwa wakihaha kuitisha mkutano wao na kupanga ufanyike kesho asubuhi katika hoteli hiyo ya Travertine, Magomeni, kabla ya jeshi la polisi kutangaza kuipiga marufuku.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...