https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, December 30, 2012

Umasikini wa Handeni waumiza wengi



Wakazi wa moja ya vijiji vya wilaya ya Handeni kama walivyopigwa picha na Handeni Kwetu hivi karibuni.



Na Mwandishi Wetu, Handeni
WAKAZI wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga wametajwa kuishi kwa umasikini unaofikia 80%, huku watu hao wakiishi kwa kipato cha sh 1000 kwa siku hali inayosababisha kuwa na maisha duni kutokana na kutotumika vyema fursa za kiuchumi zilizopo.
Hayo yamebainishwa na juzi na Katibu Tawala ya Wilaya hiyo John Tike, wakati akisoma risala ya uzinduzi wa mradi wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wa Moto wa Nyika, unaofadhiliwa na Shirika la Kazi Duniani ILO, kupitia asasi ya kiraia maendeleo ya jamii (CDMT).
Alisema idadi hiyo ni kubwa  kwa wananchi wa kawaida kupata kipato hicho hali inayosababisha kurudisha nyuma kasi ya maendeleo na umaskini kutawala kutoka na kukosa kipato cha kuweza kujikimu kwa familia.
“Tukiwatumia vijana hawa vizuri katika mradi huu wataweza kuleta ushindani wa maendeleo katika wilaya hii, ikiwa tu watajituma kwa lengo la kuleta mabadiliko kwani wao ndio chachu ya mabadiliko nchini,” alisema Tike.
Tike alisema ikiwa mradi huo watauzingatia wataweza kuboresha maisha yao na yafamilia zao kwa ujumla pia tatizo la ajira litapungua kwa kiasi kikubwa kwani sasa watakuwa wamepewa elimu ambayo watahitajika kuifanyia kazi baada ya hapo.
Nae Kaimu Mkurungezi wa Wilaya hiyo Julius Mhando alisema kuwa moja ya vipaumbele katika Halimashauri hiyo ni kuhakikisha kipato cha mtu mmoja mmoja kinakuwa kutoka 1000 ya sasa hadi kufika 3000 kwasiku .
Alisema katika kulitekeleza hilo wameanda mpango wa jamii shirikishi kwa kuunda vikundi vya watu 10 hadi 20 na kubuni mradi watakaoweza kuuendesha na Halimashauri kuwawezasha ufadhili wa mradi huo ili kujiletea maendeleo.
“Tunachokifanya ni kuunda vikundi vya nguvukazi na kuviweka pamoja  kisha kuwatafutia ufadhili wa vitendea kazi kama ni kilimo tunawatafutia pembejeo za kilimo na eneo la kulima chini ya usimamizi wa maofisa ugani,” alisema Mhando.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...