https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 15, 2012

MAMBO FULANI MUHIMU



 Tafuta muda wa mapumziko na mwenzako





Faragha ya wawili wapendanao hawa

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KUNA watu ambao licha ya kuwa na uwezo na muda wa kuweza kutoka pamoja na wapenzi wao, ila jambo hilo ni gumu zaidi kwao.

Wapo nyumba ile ile, eneo lile lile. Hata muda wa kutoka nje ya maeneo ya nyumba zao kwa ajili ya kuzungumza hili na lile na wake au waume zao hawana.

Hili nim tatizo kubwa. Ni tatizo, hasa pale mwanaume au mwanamke anapoamua kutoka peke yake au kutoka na watu wa nje.

Kwanini? Najua kuna wakati mtu anatamani kuwa peke yake, ila katika suala zima la mapenzi, kunaashiria kwamba uhusiano wao umeanza kuyumba.

Unatakiwa wewe na mtu wako kuongeza mapenzi kila wakati kama njia ya kudumisha uhusiano wenu au ndoa zenu kwa nyie mliofunga ndoa.

Huo ndio ukweli wa mambo. Jaribu kumchukua mpenzi wako na kumpeleka nje ya eneo mlilozoea siku zote. Mfano, kama unaishi Sinza, jijini Dar es Salaam, basi mkapumzike Kawe, Msasani katika beach yoyote ambayo ni chaguo lenu.

Huo sio utaratibu wa wageni. Kutembea na kufurahia sio utamaduni wa Wazungu kama wanavyofanya baadhi yao. Hapo hujaiga.

Na hata kama utakuwa umeiga utaratibu huo, hakika hujaiga tabia mbaya zisizofaa katika jamii, hasa kama umeangalia na kipato chako.

Kwa mfano, ukienda beach ya kulingana na kipato chako, au ile ya Coco Beach ambayo kila Mtanzania anaweza kwenda hapo bila malipo ni jambo zuri na linaloweza kuongeza ladha ya uhusiano wenu.

Hapo mkifika mtakaa pamoja naa kuzungumzia mustakabali wa mapenzi yenu. Mtaangalia yalipotoka na yanapokwenda.

Kama mlikwazana katika kipindi cha nyuma, hakika mtajua kosa lenu na kujisahihisha kwa nia ya kufanya marekebisho mazuri kwa ajili ya penzi lenu.

Na kama mna kipato kizuru, basi mnaweza kwenda katika hoteli zenye beach nzuri na zenye ulinzi wa kutosha. Sitaki kuzitaja, maana zipo nyingi zenye hadhi ya kuvutia.

Hapo penzi litazidi kuchanua. Mtakuwa pamoja na kuangalia kila linalopita mbele yenu, iwe baya au zuri. Hapo kila mmoja atatoa msimamo wake na namna gani mnaweza kusonga mbele zaidi.

Kwanini uende katika maeneo hayo wakati unapoanza penzi jipya huku ukishindwa kwenda tena mnapokuwa pamoja?

Nadhani kuna kila sababu ya kujiangalia upya, kama tuna lengo la kutoa dosari kwenye uhusiano wenu, maana mapenzi yana utamu wake.

Mwambie mpenzi wako. “Leo najisikia kuzungumza na wewe nje ya nyumba yetu”.

Nadhani naye atajisikia faraja kama bado anapendwa na kuthaminiwa, ukizingatia kwamba wapo wanaowafanya wake zao ni walinzi wa nyumba huku wao wakila ‘bata’ kustarehe na wapenzi wa pembeni au marafiki zao.

Tuache tabia hiyo ya ajabu na isiyokuwa na mashiko katika jamii, ukizingatia kwamba mapenzi ni mazuri kama yakihusisha wawili wapenda nao.

Tukutane wiki ijayo.

0712 053949
0753 806087

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...