https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 29, 2012

Linah sasa atamani kurudi shule



Mwanadada Lina Sanga, aakionyesha pozi alipokuwa nchini Marekani kwenyee shughuli zake za muziki.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Linah Sanga, amesema shule ni jambo jema hivyo kuna haja ya wasanii kujikita zaidi humo.

Kauli ya Linah inakuja wakati wasanii wengi kuona hakuna haja ya kuendelea na masomo zaidi ya kujikita zaidi katika sanaa kwa kuangalia mafanikio yao.

Akizungumza na Handeni Kwetu mwishoni mwa wiki iliyopita, Linah alisema uzuri wa shule ni pale muziki utakapotupa mkono, hivyo kuweza kuajiriwa popote.

Alisema kinyume cha hapo, mtu ambaye aliwekeza zaidi kwenye muziki, endapo sanaa itamtupa mkono, maisha yake yanaweza kuwa magumu zaidi na kuchanganyikiwa.

“Shule ni nzuri zaidi, natamani hata leo kuendelea kusoma huku nafanya sanaa yangu nikiwa na malengo ya leo na kesho, hasa muziki utakapokuwa tofauti.

“Hivyo wasanii twendeni shule na sio kuangalia zaidi muziki, hasa wale vijana wanaoangalia mafanikio ya watu waliotangulia na kukimbia shule,” alisema Linah.

Linah ni miongoni mwa wasanii wa kike wenye mafanikio makubwa katika tasnia hiyo huku, huku nyimbo zilizomuweka juu zikiwa ni Atatamani, Lonely na nyinginezo, wakati huo yupo chini ya taasisi ya kulea na kukuza vipaji ya Tanzania House of Talents (THT).

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...