https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 29, 2012

Arusha wapeta medani ya masumbwi



Meya wa Arusha, Gaudence Lyimo
Na Mwandishi Wetu, Arusha
JIJI la Arusha linazidi kubarikiwa baada ya kuteuliwa kuwa Makao Makuu ya Chama cha Ngumi za Kulipwa Cha Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA), huku muombaji mkuu wa jambo hilo akiwa ni Mstahiki Meya wa Arusha, Gaudence Lyimo, akiwa na lengo la chama hicho kuwa karibu na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC).
o
Rais wa ECAPBA, Onesmo Ngowi
Akizungumzia suala hilo, Rais wa ECAPBA Onesmo Ngowi, alimhakikishia meya kuwa ECAPBA itahamishia makao yake makuu katika jiji la Arusha, ikitoka katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.
Alisema kuwa Juhudi za Lyimo za kukuza michezo na kukuza utalii katika jiji la Arusha ni moja ya sababu zilizomfanya rais wa ECAPBA kuamua kuhamishia ofisi hizo katika jiji la Arusha.
“Uamuzi huo uliungwa mkono na mmoja wa wanachama wa  ECAPBA bw. Daudi Chikwanje ambaye ndiye Katibu Mkuu wa Chama Cha Ngumi za Kulipwa Cha Malawi.
“Nchi ya Malawi ni mwanachama wa ECAPBA pamoja na Kenya, Zambia, Ethiopia, Burundi, Sudan ya Kusini, DRC, Rwanda, Uganda na Sudan,” alisema.
ECAPBA inaratibu ubingwa unaojulikana kama ECAPBF ambao unawapa mabondia wa ukanda huu kuwa mabingwa imara wa ngumi Afrika.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...