https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, December 28, 2012

ADC wavuna wanachama 2700 Handeni



Na Mwandishi Wetu, Tanga.
JUMLA ya wanachama wasiopungua 2700 wamefanikiwa kujiunga na Chama kipya cha Alliance Democratic Change (ADC) wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Wanachama hao wamepatikana baada ya kufanya ziara ya kuzungumza na wananchi, kufungua matawi ya chama hicho na kusikiliza kero zao na jinsi ya kuzipatia ufumbuzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga, Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Said Miraji, alisema ziara yao walifanya kwa kushtukiza na kugundua kuwa wilaya hiyo ina kero za maji, afya na elimu.

Alishangazwa kuona wananchi wa kata mbalimbali wilayani humo wakikabiliwa na tatizo la maji ingawa wana vyanzo vitano vya maji ambavyo ni Kitumbi, Bongi, Segera Michungwani, Msilwa na Chogo.

Alisema licha ya wananchi wengi kushindwa kutapa huduma ya maji katika maeneo yao lakini Mbunge wa Jimbo hilo, Abdallah Kigoda ambaye pia ni Waziri wa Viwanda na Biashara anafanya ziara ya kutembelea Jimbo hilo huduma ya maji inapatikana lakini anapomaliza ziara yaka huduma hiyo inatoweka.

“Hii hali ya upatikanaji wa maji kwa kipindi cha ziara ya Mh Mbunge wetu inatushangaza sana sasa tunajiuliza hao watu ambao wanaleta maji wanapomuaona mbunge wanatoa wapi," alihoji.
 
Aliongeza kuwa kuanza kwa elimu ya msingi kwa kigezo cha kupitia elimu ya awali sio agizo rasmi la kitaifa kwa sababu sio wazazi wote wenye uwezo wa kuwalipia karo watoto wao katika elimu hiyo ya awali .

Hata hivyo alisema katika suala la afya alieleza lipo tatizo la kutokupewa msamaha wa kupatiwa matibabu bure wazee,wazazi na watoto wadogo kama serikali ilivyoagiza kitu ambacho kinapeleka kuleta usumbufu kwa jamii husika kwa ujumla.

Alisema katika ziara yao fupi wilayani Handeni walifanikiwa kufungua matawi yapatayo 24 katika kata za Kabuku, Kwamkonga, Handeni Mjini, Mkata, Ndolwa na Misima.

Aidha alieleza kuwa wanatarajiwa kufanya ziara rasmi kwa uzinduzi wa matawi hayo mikutano ya hadhara katika wilaya za Mkinga, Handeni na Tanga mjini lengo ni kukiimrisha chama hicho ili kuweza kuchukua dola siku zijazo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...