https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, December 30, 2012

TAARIFA KWA WAWEKEZAJI WAPYA KATIKA KILIMO CHA MITI YA MBAO, KARATASI NA NGUZO.


Wadau wakiangalia vitalu vya miti

 Fresh Farms & Tours (T), biashara tanzu ya Anesa Co.Ltd (Nyaluke Business Empire); inajishughulisha na upandaji, utunzaji na uendelezaji wa mashamba ya miti ya mbao, karatasi na nguzo-mkoani Iringa.
Vilevile inahusika na uvunaji na usambazaji wa mazao ya miti, (mbao na nguzo za umeme) sambamba na ufugaji.
Fresh Farms ilianzisha programu maalumu, mapema mwaka jana; inayolenga kuwawezesha watanzania wengine kuwekeza katika kilimo cha miti kwa urahisi.
Tayari makumi ya watanzania wamechangamkia fursa hii. Fresh Farms & Tours (T) tunapenda kuwaarifu wale wote wenye nia ya kuwekeza nasi, kuwa kuanzia Februari Mosi, 2013 kutakuwa na mabadiliko ya bei na gharama za uendeshaji kwa mashamba ya miti.
Mashamba tunayoyauza laki sita kwa sasa; bei mpya itakuwa milioni moja; na yale tunayouza laki nane gharama yake itakuwa milioni moja na nusu.
Bei hizi hazitawaathiri wateja wa awali na wale ambao wamekwisha wasilisha oda zao. Fresh Farms & Tours (T) tunaendelea kuboresha huduma, taarifa na usaidizi kwa wote wanaowekeza nasi.
Fresh Farms & Tours (T) tunakutakia heri ya Mwaka mpya wa 2013 na tunakukumbusha ile salamu yetu(motto); "Greening the world and Feeding People".
IMETOLEWA NA:
Albert Nyaluke Sanga, (SmartMind)
Mtendaji Mkuu-Fresh Farms & Tours(T),
(C) 2012

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...