https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, April 01, 2014

Mdau wa muziki Tanzania, Said Mdoe afiwa na mama yake mzazi

TAARIFA YA MSIBA: MAMA MZAZI WA SAID MDOE WA SALUTI5AFARIKI DUNIA
Marehemu Bi Desta Mohamed enzi za uhai wake.
MAMA mzazi wa mmiliki wa mtandao wa Saluti5, Said Mode -Bi Desta Mohamed - amefariki ghafla Jumatatu ya tarehe 31/3/2014 saa 1 za jioni.
Alipata homa kali Jumapili mchana, akapelekwa hospitali (IMTU) akapata matibabu na kuruhusiwa kurudi nyumbani. Hali yake haikuwa mbaya wala ya kutia mashaka.
Jumatatu akaamka vizuri na akashinda vizuri hadi saa 12 za jioni hali ipoanza kubadilika tena. Akafariki akiwa njiani kupelekwa hospitali.
Msiba uko Dar es Salaam, Mbezi Beach Old Bagamoyo Road kituo cha Zena Kawawa.
Mazishi yatafanyika Jumanne 1/4/2014 saa 10 alasiri kwenye makaburi ya Mbezi Beach (New Bagamoyo Road) mbele kidogo ya  Masana Hospital.
INNA LILLAHI WAINNA ILAYHI RRAAJIUN.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...