https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, April 25, 2014

Msemaji wa Coastal Union Hafidh Kido atangaza kujiuzuru kwenye klabu hiyo kutokana na kuzuka migogoro mizito



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MSEMAJI wa klabu ya Coastal Union yenye maskani yake jijini Tanga Tanzania, Hafidh Kido, ameachia ngazi kutokana na migogoro mizito inayoendelea kuitafuna timu hiyo iliyomaliza ligi katika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa ligi.
Msemaji wa zamani wa Coastal Union, Hafidh Kido pichani.
Akizungumza leo asubuhi jijini Dar es Salaam, Kido alisema kuwa amelazimika kujiuzuru ili kulinda hadhi yake katika sekta ya habari kutokana na mikanganyiko ndani ya timu hiyo.

Msemaji wa zamani wa Coastal Union, Hafidh Kido, akiwa katika majukumu yake.
Alisema awali uongozi wa klabu hiyo haukumpa ushirikiano katika majukumu yake, hali iliyolazimika kusaidiwa kwa kiasi kikubwa na aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu hiyo na Mfadhili wao, Nassor Bin Slum.

“Mimi Hafidh Athumani Kido, nikiwa na akili timamu natangaza kutojihusisha na shughuli zote za Coastal Union, hasa usemaji wa klabu, huku miongoni mwa sababu nyingi zilizonifanya kutangaza uamuzi huo ni sintofahamu iliyozuka ndani ya klabu yetu.

“Kwa taaluma yangu ya uandishi wa habari lazima niwe na msimamo juu ya mambo yanayoendelea kwenye jamii ili niendelee kufanya kazi na klabu hii kwa wakati huu wa misuguano, lazima niwe na upande; kwa maana upande unaounga mkono uongozi ama upande usiokuwa na Imani na uongozi,” alisema Kido. 

Kwa mujibu wa Kido, yeye ameamua kutounga mkono upande wowote, akiamini atakuwa katika mstari sahihi na kukaa pembeni ili afanye shughuli zake za uanahabari kwa furaha na amani, huku akisema kuwa ataendelea kuwa mwanachama halali wa Coastal Union Sports Club mwenye kadi 0013.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...