https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, April 19, 2014

Yanga chupuchupu kuchezea kichapo kutoka kwa Simba, Azam washinda tena


Timu ya Yanga leo imeshindwa kujibu kipigo cha mtani wake wa jadi, Simba, baada ya kutoka sare ya bao 1-1, mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Bao la Simba lilipatikana katika dakika ya 75 kupitia kwa Haruna Chanongo wakati lile la Yanga liliingia dakika ya 88 kupitia kwa Simon Msuva, katika mechi iliyokuwa na vituko vya aina yake.


Katika mechi hiyo iliyokuwa na msisimko wa aina yake, mlinda mlango wa Simba, Ivo Mapunda, hatashindwa kuisahau baada ya taulo lake kuibua kizaa zaa na kulazimika kutupwa nje na wachezaji wa Yanga, wakiongozwa na Khamis Kiiza.


Katika mechi hiyo, Yanga ndio waliokuwa na shauku ya kushinda kutokana na kushika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi, huku ikiwa na kumbukumbu ya kupigwa bao 3-1 katika mechi ya mtani jembe iliyowaacha mashabiki wake njia panda.


Awali mpira ulianza kwa kasi huku kila timu ikijipanga kushinda katika dakika za mwanzo za mchezo huo.  Timu ya Simba iliweza kumiliki vyema dakika tano za kwanza, kabla ya Yanga kuzinduka na kujibu mashambulizi ya mtani wake.


Katika mechi nyingine, timu ya Azam iliibuna na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Ruvu, mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam, hivyo kumaliza bila kufungwa sambamba na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Bara, huku bao la pekee likipatikana katika dakika ya 79 kupitia kwa Brian Umony.


Mkoani Tanga, timu ya Kagera Sugar iliweza kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union ya mkoani humo, huku bao lao likipatikana   

dakika ya 50 kupitia kwa Themi Felix, akitumia kazi nzuri ya Paul Ngwai.




No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...