https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, April 22, 2014

Uhakiki yachomoza mashindano ya nyama choma jijini Dar es Salaam



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAA ya Uwakiki iliyopo Kijichi, imeibuka kidedea  kwa kuwa baa inayochoma nyama bora katika shindano la Safar Lager Nyama Choma mkoa wa Dar es Salaam.
Iliibuka juzi katika fainali za shindano hilo zilizofanyika katika Viwanja vyaLeaders, Kinondoni Dar es Salaam na kujinyakulia kitita cha  sh.milioni moja, kombe na cheti.

Jumla ya baa sita kutoka wilaya zote Dar es Salaam, ziliingia fainali ambapo nafasi ya pili ilinyakuliwa na baa ya Meedakutoka Sinza, ambayo iliondoka na sh.800,000 , ikifuatiwa na Dar Safari Park iliyopata
600,00, Soccer City,400,000, Fyatanga 200,000 na Blue Fish, 100,00.

Pamoja na  zawadi za fedha, pia baa hizo zilipata vyetivya ushiriki, ambapo bendi  ya Twanga Pepeta na disko la DJ John Dilinga 'JD', viliongoza burudani katika fainali  hizo.

Awali akizungumza katika shamrashamra hizo, Meya wa Manispaa Kinondoni, Yusuf Mwenda alisema shindano hilo likitumika vizuri, linaleta afya bora na kuongeza ajira kwa vijana.

"Shindano hililinasaidia kuweka afya yamlaji nyama salama, nahivyo kuongezaidadu yawalaji,kupanuasoko la biashara ya nyamana hatimayemfugaji kufaidika na ajira kuongezeka,"alisema.

Meneja  wa Bia ya Safari, OScar Shelukindo alisema wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha maendeleo kwenye jamii kupitia udhamini wa michezo pamoja na uwezeshaji wa wafanyabiashara.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...