https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, April 27, 2014

Mashali avunja mazoezi ya kumuwinda Nyilawila

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam


BONDIA Thomas Mashali, amesema kwamba amesimamisha mazoezi kwa muda ya kumkabiri Kalama Nyilawila baada ya kupata ajali ya gari, ila bado si tatizo la yeye kuweza kumvaa Nyilawila na kumuonyesha adabu. 

Bondia Thomas Mashali pichani.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mashali alisema kuwa ana uhakika wa kumpiga Nyilawila ingawa pambano hilo limesogezwa mbele hadi litakapotangazwa tena na promota wao Ally Mwazoa.


Alisema ajali aliyoipata si kubwa ingawa imemfanya asimamishe mazoezi kwa siku kadhaa kwa ajili ya kuvaana na Nyilawila katika pambano lao.


“Nilipata tatizo kidogo la ajali lakini naamini ni changamoto zitakazonifanya nijiandaye vyema.


“Ushindi kwangu dhidi ya Nyilawila ni muhimu na lazima apigwe kwasababu uwezo wangu ni mkubwa,” alisema.


Kwa mujibu wa Mashali, pambano hilo limesogezwa mbele hadi litakapotajwa tena, hivyo kwake yeye itakuwa ni sehemu ya kujiandaa vizuri.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...