https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, April 25, 2014

Mwandishi ageukia muziki wa injili



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWANDISHI mwandamizi wa habari nchini, George Kayala yupo katika hatua ya mwisho ya kukamilisha albamu yake ya nyimbo za injili akiwa chini ya leo ya Best Record inayoongozwa na Mkurugenzi, Benjamin Nzogu.

George Kayala, mwandishi aliyeingia katika muziki wa injili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kayala alisema kwa muda mrefu amekuwa na kiu ya kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji na wakati umefika na anatarajia kuachia kibao kimoja wiki ijayo ambacho kitaanza kusikika kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini.

“Kila jambo na wakati wake, binafsi nimekuwa na kiu ya kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji kwa muda mrefu lakini sikufanya hivyo kwa sababu nilikuwa nasikiliza sauti ya Roho Mtakatifu na sasa ameruhusu nifanye hivyo, hivyo albamu yangu itakuwa tayari muda wowote kuanzia sasa,” alisema Kayala.

Kayala alizitaja nyimbo hizo kuwa ni Siwema, Usinipete, Wamebeba Matatizo,  Jehova Yile, Safisha Moyo Wangu,  Wanijua Vema Bwana na  Unayejibu kwa Moto na mpaka sasa hajapata jina la albamu kutokana na kila wimbo kuwa na sifa ya kubeba albamu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...