https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 03, 2014

Asha Baraka awapiga vijembe wapinzani wake



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa bendi ya The African Stars, Twanga Pepeta, Asha Baraka, amewapiga vijembe wapinzani wake, akisema kuwa wamekuwa wakiuchunia ukumbi wa Club Billicanas kwasababu ni mgumu kwao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Asha alisema hiyo ndio sababu ukumbi huo, unakimbiwa na bendi nyingine zisizokuwa na uwezo wa kuwavuta mashabiki wao popote walipokuwapo.

Alisema hiyo ndio sababu ya bendi yao kuendelea kutamba katika tasnia ya muziki wa dansi nchini, huku akisema wataanza kufanya mambo upya katika ukumbi huo kuanzia leo Jumatano.

“Bendi yetu haijakuwapo Billicanas kwa zaidi ya miezi miwili, lakini hakuna aliyejaribu kuuchukua ili wapige wao siku za Jumatano, badala yake waliufungia vioo.

“Hivyo kuamua kurudi pale ni kuonyesha kuwa Twanga ndio bendi pekee inayoweza kufanya shoo katika maeneo yote na watu wakahudhuria, hivyo huu ni wakati wa kuonyesha ubabe wetu katika muziki wa dansi,” alisema.

Shoo ya Twanga Pepeta leo itakuwa ya kwanza kwa vijana hao tangu waliporejea katika ziara zao za mikoani, ambapo walitembelea mikoa ya Njombe, Ruvuma na  Mbeya.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...