https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, April 01, 2014

Pambano la Cheka, Mrusi lasogezwa mbele

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
PAMBANO la Francis Cheka na Varely Brudov wa
Russia lilililokuwa lifanyike Aprili 5 jijini Dar es Salaam limesogezwa mbele hadi litakapotangazwa tena,  lile la Francis Miyeyusho na Ronald Pontillas wa Ufilipino likibaki palepale.


Promota wa pambano hilo, Mussa Kova, pambano la Cheka limesogezwa baada ya Brudov kuvunjika mguu akiwa mazoezini hivyo kutakiwa kutopigana kwa wiki mbili kuanzia Ijumaa iliyopita.  Kova alisema Brudov aliteleza wakati akiwa gym kujiandaa na pambano na Cheka la kuwania ubingwa wa dunia wa WBF kwenye uzani wa light heavy lililopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam.


"Baada ya kupokea taarifa ya kuumia kwa Brudov, tuliwasiliana na Rais wa WBF ili tubadilishiwe bondia na WBF walituambia kama bondia atabadirika pambano halitakuwa la ubingwa wa dunia. "Kwa kuwa lengo letu ni kuandaa mapambano yatakayowasaidia mabondia wa Tanzania kupanda kimataifa tuliamua kuliharisha kwa muda hadi Brudov atakapopona ingawa pambano la Miyeyusho na Pontillas litafanyika siku hiyo ya Aprili 5 kwenye ukumbi wa PTA," alisema Kova.


Akizungumzia pambano la Miyeyusho, Kova alisema maandalizi yanakwenda vizuri na kusisitiza kuwa litasimamiwa na chama cha ngumi za kulipwa Tanzania (PST).
"Mabondia wote wako katika hali nzuri ya ushindani, tunategemea Miyeyusho atafanya vizuri na kukabiliana na upinzani wa mpinzani  wake kwani ni bondia mzuri na mwenye kiwango cha juu," alisema Kova.


Katibu mkuu wa PST, Anthony Lutha alisema kama chama wamekamilisha taratibu zote za maandalizi ikiwa ni pamoja na kutoa kibali cha pambano hilo ambalo awali lilitajwa kusimamiwa na TPBF chini ya rais wake, Chatta Michael. "Tunamtaki Miyeyusho maandalizi mema kwani mabondia wa Ufilipino ni wazuri na wanakiwango kikubwa katika masumbwi, hivyo Miyeyusho ajifue kwelikweli ili kumkabili na kutwaa ubingwa," alisema Lutha.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...