https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, April 05, 2014

TAZARA wapinga vifaa bandia vya Simba



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KATIBU mwenezi wa tawi la Simba la TAZARA lenye maskani yake jijini Dar es Salaam, Alfred Mdemu, amesema kwamba watawashawishi wanachama wao wanaotokea katika tawi lao kujilinda na ununuaji wa vifaa vya michezo vyenye nembo ya Simba ambayo ni batili.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mdemu alisema katika kulifanyia kazi suala hilo, kila mwanachama wao lazima anunuwe vifaa hivyo mahali panapojulikana au kuagizwa kwa pamoja kutoka sehemu husika.

Alisema kununua jezi ya Simba ambayo ni bandia hakuwezi kuisaidia klabu hiyo kwakuwa fedha zao zinakwenda kwa wafanyabiashara wachache wasiokuwa na malengo ya kuiletea mafanikio klabu yao hiyo yenye maskani yake jijini Dar es Salaam.

“Kuanzishwa kwa matawi ya Simba kuende sambamba na kufanikisha maendeleo kwa kuhakikisha kuwa wanachama wananunua vifaa halali vya michezo, zikiwamo jezi ambazo timu nyingi ndio biashara halali.

“Kwa sisi TAZARA tunajipanga kuona namna gani tunanunua vifaa halali tukiamini ndio klabu yetu itaingiza fedha nyingi badala ya kununua kwa watu ambao sit u hawatambuliki, bali pia vifaa vyao vinakuwa vya bandia,” alisema Mdemu.

 Tawi la Simba TAZARA lina wanachama 176, huku likiwa na mipango kabambe ya kuhakikisha kuwa ujio wao huo unakuwa na tija kwa klabu yao inayoongozwa na Ismail Aden Rage kwa sasa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...