https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 03, 2014

Simba waapa kufia uwanjani kusaka heshima



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UONGOZI wa klabu ya Simba SC, umesema ingawa wapo kwenye nafasi ngumu kuwania nafasi ya tatu ya msimu wa Ligi, ila wataendelea kujipinda hadi dakika ya mwisho, ili waone wamevuna jambo gani kwa manufaa ya timu yao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Msemaji wa Simba, Asha Muhaji, alisema bado hawajakata tamaa katika ligi ya Tanzania Bara, ingawa bado hali imeendelea kuwa mbaya kwa upande wao.

Alisema benchi la ufundi na wachezaji wao wamekuwa wakifanya bidii, ila matokeo mabaya hayawakatishi tamaa ya kuendelea kusaka heshima ya klabu yao, ingawa alikiri kuwa mambo yatakuwa magumu kutokana na ushindani uliopo katika kuelekea mwisho wa Ligi ya Tanzania Bara, inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania.

“Mechi yetu na Azam ilimalizika kwa kushuhudia tukifungwa bao 2-1 ila bado hatujakata tamaa ya kuendelea kupigania nafasi za juu, ingawa juu ya ubingwa inaonekana dhahiri kuwa tumejitoa katika mchakato huo,

“Lolote linaweza kutokea katika kuelekea mechi za mwisho za ligi ya Tanzania Bara, hivyo naamini vijana wetu wataendelea kupigania heshima ya timu yao ya Simba,” alisema,

Kufanya vibaya kwa timu ya Simba, kumepokewa vibaya na mashabiki wao, hali inayowafanya waelekeze nguvu zao kuishangilia Azam FC, wakiwa na maana ya kuwabeba ili mtani wao wa jadi, Yanga asiweze kutwaa taji hilo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...