https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, April 27, 2014

Twanga Pepeta kupagawisha Leaders Club leo


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

BENDI ya The African Stars, Twanga Pepeta, leo itawaonyesha kazi mashabiki wao katika Viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam katika onyesho lao la  bonanza linalofanyika kila Jumapili.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Meneja wa bendi hiyo, Hassan Rehani, alisema onyesho hilo lina mvuto wa aina yake.

Alisema mashabiki wao hupata nafasi ya kuburudisha mashabiki wao kuanzia saa nane mchana hadi saa nne usiku.

“Bonanza la kila Jumapili hutoa fursa kwa mashabiki wote kufurahia burudani za Twanga Pepeta. 
“Tunaamini tutaendelea kuwa pamoja na mashabiki wetu ili kulinda heshima yetu katika muziki huu,” alisema.

Twanga Pepeta ni miongoni mwa bendi zenye mashabiki wengi katika kona ya muziki wa dansi nchini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...