https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 23, 2014

Waliotimuliwa uanachama Yanga waendelea kufungiwa vioo



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Uongozi wa Klabu ya Young Africans umeshangazwa na taarifa zilizoandikwa kwenye mojawapo ya vyombo vya habari juu ya Wanachama wa Tawi la Tandale kusema hawatambui kufutwa kwa Tawi lao.


Taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari na kusainiwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, ilisema kuwa mnamo Mei 04, 2014 Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji alitangaza kulifuta tawi hilo. Alisema uamuzi huo ulikuja baada ya tawi hilo la Tandale kutokana na kua chanzo cha migogoro ndani ya klabu kwa kipindi cha mrefu.


Alisema kufutwa kwa tawi la Tandale unatokana na kutotimiza idadi ya wanachama mia moja (100)  kama inavyojieleza kwenye Katiba ya Yanga SC, Ibara ya 6, kipengele cha 4

Alisema kuwa kutakuwa na uundaji wa matawi katika maeneo mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi, huku kiwango cha chini ya idadi ya wanachama ambao wanaweza kunda tawi kisipungue watu mia moja (100).


“Ibara ya 13, kipengele cha 2 kinasema " Kutolipa ada zake za uanachama kwa muda wa miezi sita mfululizo bila ya sababu maalum inayokubalika na Kamati ya Utendaji"

“Baadhi ya Wanachama  walijifuta uanchama wao kutokana na kushindwa kulipia ada zao za uanachana kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita, kama inavyojieleza kwenye Katiba kwamba mwanachama asipolipia ada yake zaidi ya miezi sita moja kwa moja anajifuta uanachama wake,” alisema.


Hivyo uongozi wa klabu ya Yanga SC unaomba umma na wanachama wake duniani kote watambue kuwa tawi la Tandale lilifutwa kwa kutokana na kutokidhi vigezo, huku wanachama wengine sita  wakijifuta uanachama kwa kushindwa kulipia ada zao kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita.


Mwisho wanachama wa klabu ya Yanga SC wanaombwa kulipia ada zao za uanchama mapema kabla ya muda wao kumalizika ili waweze kushiriki mkutano mkuu wa marekebisho ya katiba utakaofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi - Oysterbay Juni Mosi 2014.



No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...