https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, May 29, 2014

Uchaguzi Mkuu Simba moto wawaka, TAKUKURU waingia kwa fujo zote

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Uchaguzi Mkuu Simba umeanza kuibua hofu baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kuanza kuufuatilia kwa karibu uchaguzi huo utakaofanyika Juni 29 mwaka huu, jijini Dar es Salaam, baada ya maofisa wa taasisi hiyo kuvamia bwalo la maofisa wa Polisi, jijini Dar es Salam, wakati wa usaili wa wagombea.


Kuingia kwa maofisa hao, kumekuja huku uchaguzi wa Simba unaotarajiwa kufanyika Juni 29 mwaka huu ukizidi kupamba moto na kila mmoja kuwa na imani na mgombea wake kuwa ataibuka na ushindi.


Katika uchaguzi huo, nafasi ya urais inawaniwa na Evans Aveva na Andrew Tupa,  huku Michael Wambura akitupwa nje hivyo kusubiri uamuzi wa Kamati ya Rufaa ya Shirikisho la Soka nchini (TFF).


Mbali na urais, Swed Nkwabi na Godfrey Kaburu wanachuana vikali, ambapo makundi ya wagombea hao wanaendelea kuchuana, huku kambi ya Nkwabi, inaonekana kuwa na nguvu zaidi ya Kaburu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...