https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, May 27, 2014

Mike Mwakatundu aja na mpango mzuri wa sanaa na wasanii Tanzania

TATIZO = FURSA
ukiijua hiyo hesabu vizuri maisha kwako yatakuwa bam bam

Wasanii wengi kwa kipindi kirefu tumekuwa tunalalamika kuwa tunabaniwa kwenye MEDIA bila kuelewa kwa kifupi tu ukweli wa mambo.

Kwa Uchunguzi nilioufanya kwa kipindi cha miaka mitatu hivi nimegundua haya, Watayarishaji au watangazaji wa vipindi kwa siku wanapokea zaidi ya nyimbo 30 kutoka kwenye studio mbalimbali hapa nchini, kwao inakuwa ni vigumu kucheza nyimbo zote kutokana either muda kuwa mdogo wa vipindi vyao au kuwa na request nyingi za nyimbo ambazo wamekuwa wanazicheza sana.
Swali likaja kwangu nyimbo au video ambazo hazichezwi na ni nzuri
tufanye nazo nini ili na hawa wasanii wapate airtime?

SULUHISHO LA TATIZO
Baada ya kuliona tatizo nikapata idea ya kuzunguka kwanza Manispaa zote ILALA, KINONDONI na TEMEKE kuangalia usajili wa vituo vya bodaboda na bajaj zilizosajiriwa kwenye vituo ambazo pia wameweka radio ambazo zinatumia flash na memory cards,
Huku nikapata idea ya kuanzisha KITAA RADIO ambayo itahusika na kuwasambazia watu hapa muziki ule ambao ulishindwa kupenya radioni muziki wa aina yeyote wa Kitanzania ambao mzuri kusikika na watu wakaupenda.

Pili, kwenye upande upande wa video napo nikajiuliza ni mabus mangapi yaendayo mikoani ambayo ndani hutoa burudani ya movies , music video nk nikakuta ni zaidi ya mabus 2000 ,ambapo kwa siku kila bus linasafirisha si chini ya abiria 50
Huku nako nikapata idea ya kuanzisha KITAA Television ambayo itakuwa inatoa burudani ya music videos zile tu zilizokosa kupewa Airtime kwa namna moja au nyingine

Mfanp mzuri umekuwa kwenye nyimbo ya MWANAFA ft G NAKO inakwenda kwa jina MFALME imefanya vizuri sana mtaani na kwenye radio imeanza kwenda vizuri sababu ya KITAA RADIO

Kwa kusema hayo machache napenda kusema KITAA RADIO na KITAA TELEVISION imezinduliwa rasmi now chini ya kampuni ya SHOWBIZ DEFINED MEDIA Co LTD

NB ; Huduma hii tutaitoa lakini kutakuwa na uchangiaji wa huduma kwa wale watakaokuwa tayari
Aksanteni

Mike Mwakatundu
Marketing Manager
ShowBiz Defined Media Co. Ltd
showbizdefined@gmail.com

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...