https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 30, 2014

Wabunge wa upinzani wasusa tena vikao vya Bunge, watoka nje kuacha kuijadili bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini



Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Wabunge wa Upinzani, leo wameendeleza mchezo wao wa kususa na kutoka nje ya vikao vya Bunge, kwa madai kuwa muda wa kujadili Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ni mdogo.
Wabunge wa upinzani wakati wanatoka nje ya Bunge, wakati bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini inajadiliwa.

Kauli ya kuwataka wabunge wa upinzani watoke ilitoka kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, ambaye pia ndio mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kutoka kwa wabunge hao wa upinzani kumekuwa kawaida sasa, jambo ambalo huenda likapokewa vibaya na Watanzania.

Akizungumzia hilo mjini hapa mara baada ya kutoka nje ya Bunge, Spika wa Bunge, Anne Makinda, alisema kuwa muda wa kujadili vikao vya Bunge la bajeti linaloendelea ulishawekwa, ikiwa ni baada ya Bunge la Katiba kula muda wao mwingi.

Wakati wabunge hao wanatoka nje, kauli za kejeli na dharau dhidi yao zilisikika, ikiwa ni pamoja na waache watoke, warudishe posho na nyinginezo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...