https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 30, 2014

Nay wa Mitego: Nakula Ujana unanipa raha kupita kiasi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa Hip Hop, Emmanuel Elbariki maarufu kama Ney wa Mitego, amesema wimbo wake wa ‘Nakula Ujana’ unampa raha kutokana na kupokewa kwa shangwe na mashabiki wa kizazi kipya nchini.
Msanii Ney wa Mitego pichani.
Ney wa Mitego aliyasema hayo katika mazungumzo ya kuelezea namna gani amejiwekea mikakati ya kulinda hadhi na uwezo wake kisanaa jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku chache baada ya uzinduzi wa huduma mpya ya Kampuni ya Simu za Mikononi ya Airtel Tanzania, inayojulikana kama switch on, katika Hoteli Kilimanjaro Kempisk, inayotoa urahisi wa wateja wao kupata huduma ya internet kwa urahisi.

Alisema kuwa wimbo wake huo wa Nakula Ujana umetokea kupendwa na wengi, hasa anapokuwa katika maonyesho mbalimbali, hivyo kuonyesha kuwa maendeleo yake kisanaa yamekuwa mazuri kupita kiasi.
“Nawashukuru wadau wangu wote kwakuwa wanapenda kazi zangu, hasa huu wimbo wa Nakula Ujana, ambao mimi mwenye unanipa raha.
“Naamini kila kitu kitakuwa kizuri zaidi kwa kuwapatia raha mashabiki wangu wakati wowote, kwakuwa bado nitaendelea kupambana ili kufanya vizuri zaidi katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini,” alisema.
Katika uzinduzi huo wa huduma ya Airtel, watu mbalimbali walialikwa, sambamba na msanii Barnabas na Vanessa Mdee nao kuwa miongoni mwa wasanii waliokutana kwa pamoja katika tukio la aina yake.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...