https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, May 28, 2014

Taifa Stars kuifuata Zimbabwe kesho na watu 30



NA KAMBI MBWANA, DAR ES SALAAM
MSAFARA wa watu 30 wa Taifa Stars unaojumuisha wachezaji, benchi la ufundi na viongozi unaondoka leo kesho alfajiri ya Mei 29 mwaka huu kwenda Harare, Zimbabwe kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika.

Mechi hiyo itachezwa Juni Mosi mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare, ambapo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itatua jijini humo saa 5 asubuhi na ndege ya Kenya Airways.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura, alisema kuwa msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Rais wake Jamal Malinzi, ambapo utarejea nchini Juni 2 mwaka huu.

“Wakati huo huo, mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Malawi (Flames) iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 8,380,000 kutokana na watazamaji 1,504 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo,” alisema Wambura.

Kwa mujibu wa Wambura, mgawo ulikuwa ni kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 1,278,305.08, gharama za kuchapa tiketi sh. 225,600, gharama za uwanja sh. 1,031,414.24, gharama za mechi sh. 1,375,218.98 na TFF/Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 4,469,461.69.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...