https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, February 28, 2013

TIFU TIFU: Michael Wambura azidi kumng'ang'ania Tenga kwa kumtaka aitishe Uchaguzi Mkuu wa TFF haraka


Umemuona jamani Tenga?? Hapa anawaonyesha wanahabari gazeti lilioandika habari za kujiuzulu kwake mwaka 2001....
 

Na Rahimu Kambi, Dar es Salaam
KATIBU Mkuu wa kilichokuwa Chama cha Soka TFF sasa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Michael Wambura, amesema endapo Tanzania itafungiwa na Shirikisho la Mpira la Dunia (FIFA), wa kustahili kulaumiwa ni Leodgar Tenga, Rais wa Shirikisho hilo.

Wambura alimataka Tenga aitishe mkutano badala ya kufurahia ujio wa viongozi wa FIFA, ikiwa ni njia ya kutaka Tanzania ifungiwe jambo ambalo likitokea, Watanzania watalia na Rais huyo aliyemaliza vibaya muda wake wa mwisho.

Aidha, Wambura aliitaka TFF na Kamati zake zote kuwa ziitishe Uchaguzi Huru, kabla ya kumaliza muda wake kwa mujibu wa sheria, huku akisema kuwa uamuzi wa serikali unapaswa kuungwa mkono maana umekuja kumaliza tatizo, hivyo wanaona kuwa Tanzania itafungiwa basi wa kulia naye ni Tenga.

Baada ya Serikali kupitia kwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kutangaza kutoitambua Katiba ya TFF ya mwaka 2012, Tenga aliitisha kikao cha Kamati ya Utendaji kinachotarajiwa kufanyika mwisho mwa wiki.

Michael Wambura, akionyesha kipande cha gazeti kwa wanahabari, ambalo mwaka 2001 liliandikwa juu ya kujiuzulu kwa Leodgar Tenga Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), wakati huo ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kama ushahidi wa kigeu geu chake anapokuwa kwenye uongozi.....
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...