https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, February 22, 2013

Tanzania yafanya vyema kwenye mashindano ya mitindo Uingereza

Wabunifu mitindo Jackline Kibacha na Anna Lukindo wakisindikizwa na Mama Balozi Joyce Kallanghe na Mama Rose Kiondo.
Nje ya Jumba la Somerset.
Wanamitindo wa Kitanzania kwenye London Fashion Week 2013. Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha.
Mama Rose Kiondo, Samson Soboye, Mama Joyce Kallaghe, Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha.
Anna Luks.
Anna, Jack na Duane kutoka Jamaica.
Barabara ya The Strand copy.
London Fashion Week 2013. (Picha zote za Urban Pulse).
Imeandikwa na Urban Pulse na Freddy Macha
Jumapili mchana wilaya ya Westminster jijini London ilikuwa na mashindano ya ubunifu na urembo katika maonyesho ya kimataifa ya London Fashion Week. Mashindano haya yalifanyika jumba la Somerset lililosimama imara kwenye upembe wa kaskazi ya mto Thames.
 
Maonyesho ya London Fashion Week, bado yanaendelea jumba hili la Somerset toka tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. 

Magwiji na mapapa wa mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda. Wote hukutana katika maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa biashara.
Siku hii Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na British Council na LFW kushiriki kwenye mashindano ya kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo. 

Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na Christine Mhando ndio wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka 27 sasa.
Katika kuunga mkono maendeleo ya Tanzania na Watanzania, Ubalozi wetu Uingereza na Bodi ya Utalii Tanzania, nao pia walichukua nafasi hii kuwasaidia wananchi hawa kufanikisha mahitaji yao ya ushindani. 

Ubalozi umetoa Ukumbi wa Nyumba Ya Tanzania ulioko Bond Street ili wasanii hao waweze kuonyesha nguo na sanaa zao kwa juma zima kama sheria za London Fashion Week zinavyoamuru. Vile vile Bodi ya Utalii ya Tanzania imesaidia katika mchango wa mali ghafi zilizotumika katika shughuli hizi ili kuiuza Tanzania kimataifa.
 
Mshindi wa tukio alikua Estonia. Ingawa Tanzania haikuwa mshindi wa mwanzo- ilichaguliwa kati ya Kumi Bora jambo ambalo limetikisa nyoyo na vichwa vya waandaaji, wabunifu,wafanya biashara na watafuta vipaji vya kimataifa. Hii ni mara ya kwanza kwa taifa letu kushiriki katika shughuli na wote wameguswa na kupumbazwa na usanii wa hali ya juu ulioonyeshwa na wasanii watatu wa Kitanzania. 

Lukindo, Mhando na Kibacha wamechukua nafasi waliyopewa kwa mikono miwili na wote wameisogeza Tanzania hatua moja zaidi ndani ya ulingo wa kimataifa na katika biashara hii ya mavazi na urembo ambayo inasemekana ina thamani ya Pauni Billioni 10 ama shilingi Trillion 25 za Tanzania.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...