https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, February 12, 2013

TFF kimenuka, TASWA wafuta mdahalo wa wagombea

Katibu Mkuu TASWA, Amiri Mhando

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kimefuta wazo la kuendesha mdahalo kwa wagombea wa  nafasi za juu za uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Akizungumza na Handeni Kwetu jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando, alisema kuwa mdahalo huo ulikuwa ufanyike Februari 15, 2013 na tayari chama kilikuwa katika hatua nzuri ya mazungumzo na wadhamini pamoja na kituo kimoja cha televisheni kwa ajili ya kurusha 'live' tukio hilo, ambapo kesho ilikuwa tutangaze utaratibu mzima wa  mdahalo huo.

Alisema katika mazungumzo ya leo na uongozi wa kituo hicho ambao hautaki tukitangaze, tumekubaliana kufuta wazo la mdahalo kwa  sababu nafasi ya urais amebaki mgombea mmoja, hivyo mdahalo hautakuwa na tija.

“Dhamira ya awali ya kufanya mdahalo ilikuwa kuwapa fursa wapiga kura wasikie vyema sera za wagombea urais na Makamu wa Rais, ili wananchi wawasikilize wagombea hao na pia wapiga kura wawatambue vizuri.

“Hata hivyo TASWA itatafuta utaratibu mwingine mzuri ambao utawezesha wagombea kuzungumza na waandishi wa habari na kuulizwa maswali mbalimbali ambayo tunaamini kwa kiasi fulani yatasaidia wapiga kura katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu,” Alisema.

TASWA imekuwa ikifanya mdahalo kwa wagombea wa nafasi za juu kwenye uchaguzi wa TFF, ilifanya hivyo mwaka 2001 na mwaka 2004 ingawa haukuwa wa live, ikafanya wa live mwaka 2008, ambapo yote ilikuwa ya mafanikio makubwa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...