https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 14, 2015

Wadau wa soka wamlilia kocha Sylvester Marsh

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WADAU mbalimbali wa sekta ya mpira wa miguu wamekipokea kifo cha aliyekuwa kocha msaidizi wa timu ya Taifa (Taifa Stars),  Sylvester Marsh, kilichotokea leo asubuhi.
Marehemu Sylvester Marsh, enzi za yhai wake.
Taarifa za msiba huo zimetokea huku Marsh akiwa ni miongoni mwa wadau wa  michezo na kocha mwenye uwezo na kipaji cha aina yake cha kufundisha soka. Mchezaji wa timu ya Azam FC, Himid Mao, aliandika kwenye mtandao wake wa facebook kuwa Tanzania imempoteza mtu muhimu kwenye sekta ya mpira wa miguu Tanzania.

Kocha huyo (Marsh) alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya koo na hivi karibuni alisafirishwa kutoka Mwanza hadi jijini Dar es Salaam kwa ajili yaa kupatiwa matibabu kwenye Hospitali hiyo ya Taifa.

Hata hivyo, suala la afya yake liliendelea kuwa siri kubwa huku baadhi ya wadau wakishindwa kupataa habari za uhakika zilizokuwa zinamuhusu kocha huyo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...