https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 14, 2015

Simba yainusa Yanga na Azam kwa kuwachapa Mtibwa Sugar bao 1-0

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Timu ya soka ya Simba, leo imeendeleza wimbi lake la ushindi kwa kuwafunga Mtibwa Sugar bao 1-0 katika mechi kali iliyokuwa na msisimko wa aina yake. Bao la Simba la pekee liliwekwa kimiani na mshambuliaji wa Kimataifa, Emmanuel Okwi  ‘mtaalamu’.

Kwa ushindi huo, Simba sasa imefikisha pointi 29, nyuma ya Azam FC yenye pointi 30 na Yanga ikishika usukani wa ligi hiyo kwa kuwa na pointi 31. Ushindi huo huenda ukapokewa kwa shangwe na wadau na mashabiki wa timu hiyo iliyoanza ligi kwa kusua sua.

Simba imeibuka na ushindi huku baadhi ya wadau wake wakiwa hawana imani na timu yao, licha ya kuibuka pia na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo uliowakutanisha na watani wao wa jadi, Yanga, mechi ilyochezwa hivi karibuni.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...