https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 21, 2015

Bondia wa Tanzania, Class Mawe apoteza pambano lake nchini Namibia

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BONDIA Ibrahim  Class Mawe pichani mwenye rekodi ya namba moja nchini Tanzania na namba 216 kwa Dunia  amepoteza mpambano wake wa kwanza nchini Namibia kwa kupigwa kwa pointi na bondia Julius Indongo mwenye rekodi ya Namibia ni namba moja na duniani ni namba 76 kwa ubora.
Mpambano huo uliofanyika Machi 20 katika Ukumbi wa jijini Windhoek Country Club Resort, Windhoek, Namibia ulianza kwa kasi ya ajabu ambapo bondia Class alimkalisha chini Indongo na kuhesabiwa na mpambano kuendelea kwa mashambulizi ya zamu kwa zamu kila upande hata hivyo mpaka mwisho wa mchezo Class alipoteza mpambano huo kwa pointi

Mpambano huo ni wa pili kwa Class kucheza nje ya nchi baada ya ule wa kwanza kupigana nchini Zambia mwaka jana na kurudi na ubingwa wa WPBF Africa kabla ya kuchaguliwa kwenda kupigana nchini Namibia. Pia Class alimdunda bondia Cosmas Cheka na kunyakuwa mkanda wa U.B.O Africa na kumfanya amiliki mikanda miwili ya Africa.

Mpambano huo anaupoteza baada ya miaka mitano iliyopita kuwapiga mabondia mbalimbali Class anaenolewa na jopo la makocha linalongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' Kondo Nassoro pamoja na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye umpa ushauli anapokuwa uringoni jinsi ya kukabiliana na mpinzani anaecheza nae

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...