https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, March 17, 2015

Bondia Francis Cheka abadilishiwa adhabu, sasa kutumikia kifungo cha nje badala ya miaka mitatu jela

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
BONDIA maarufu wa uzito wa juu Tanzania, Francis Cheka, pichani, amepata ahueni baada ya kubadilishiwa kifungo kutoka kifungo cha miaka mitatu jela hadi kutumikia kifungo cha nje.

Taarifa kutoka mkoani Morogoro zinasema sasa bondia huyo atatakiwa kufanya kazi katika taasisi za kiserikali kwa muda atakapokuwa anatumikia kifungo  cha nje, akitokea gerezani.

Cheka alihukumiwa kwenda jela kwa miaka mitatu baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga meneja wa baa yake Bahati Kabanda, mkoani Morogoro kwa madai kuwa ya kutoridhishwa na mahesabu kwenye biashara yake hiyo.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...