https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, March 12, 2015

Taasisi ya UWF yatoa msaada Hospitali ya Ocean Road

 Mwenyekiti wa Unity Women Foundation (UWF), Maryam Ajmy akiwa akikusanya misaada waliyokuwa wakitoa katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam kutoa msaada kwa wanawake ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanyika hivi karibuni.  
Mwenyekiti wa Unity Women Foundation (UWF), Maryam Ajmy akiwa na wanaumoja wenzake wakiingia hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam kutoa msaada kwa wanawake ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanyika hivi karibuni.   
---
Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Unity Women Foundation (UWF), umetoa msaada kwa wanawake wagonjwa katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na baada ya kutoa msaada katika Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika hivi karibuni, Mwenyekiti wa UWF, Mariam Shamo amesema wanawake wanatakiwa kujitoa kwa wanawake wenzao wenye matatizo kwa siku zote kutokana na kuwepo kwa wanawake wengine hawana msaada wa mtu yeyote.
Mariam amesema wanawake siku ya wanawake itumike kwa kwa kufariajiana na kuendelea na kuweza kuona kuona mabadiliko na kuweza kutatua changamoto zetu zinazotukabiri.Amesema wanawake wenye uwezo wasaidie na kuwatembelea wanawake wenzao katika wodi mbalimbali na kutoa msaada hata kama ni kidogo lakini kinathamani yake.
Aidha amesema kama UWF wataendelea kutoa kuwafariji wagonjwa kila muda ili nao waweze kujua wanawake wa nje yao wanatambua matatizo yao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...