https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, March 18, 2015

DC asema ujenzi wa maabara shule za kata wilayani Kilindi mambo mazuri

Na Mwandishi Wetu, Kilindi
MKUU wa Wilaya Kilindi, DC Selemani Liwowa, amesema kwamba wilaya yake ipo katika hatua nzuri juu ya ukamilishaji wa suala la ujenzi wa maabara, tangu walivyoanza mchakato huo mwaka jana.

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Selemani Liwowa, pichani.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi wilayani Kilindi, DC Liwowa alisema kwamba shule nyingi zimeshakamilika kwa kiwango cha asilimia 100, huku zile zilizosalia zikiwa katika hatua ya mwisho za (finishing), jambo linalotia moyo.

Alisema kwamba akiwa kama DC wa Kilindi alihakikisha kwamba agizo la Rais Jakaya Kikwete juu ya ujenzi wa maabara linafanikiwa kwa vitendo, hivyo kuanza kulisimamia kwa nguvu zote kwa kushirikiana na watendaji, watumishi na wananchi wote.

“Kidogo sisi tunaendelea vizuri na ujenzi wetu wa maabara ambapo shule nyingi zimefikia hatua nzuri na nyingine zilizosalia zimeshakamilika kwa asilimia zote kutokana na nguvu kazi na ushirikiano wa watu wote katika wilaya yetu.

“Naamini kwa hatua hii ile dhana ya ujenzi wa maabara itakuwa na mashiko kwa kuhakikisha kwamba shule za kata zilizosalia ambazo ujenzi wake haujakamilika unafanyika nguvu na jitihada kubwa kukamilisha mchakato huu muhimu,” alisema.

Licha ya mabadiliko kadhaa katika wilaya mbalimbali kwa wakuu wake wa wilaya kuhamishwa, DC Liwowa ni kati ya wale waliobakizwa kwenye vituo vyao vya kazi, jambo linalomfanya aendelee na program zake alizokuwa akizifanya kwenye wilaya ya Kilindi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...