https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, December 01, 2013

Siku ya Ukimwi duniani, Wanaume wilayani Handeni waaswa kupima afya zao ili kupambana na ugonjwa Ukimwi



Na Kambi Mbwana, Handeni
WANAUME wametakiwa kujenga tabia ya kucheki afya zao badala ya kuwaachia akina mama peke yao, ikiwa ni njia ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi uliozimishwa leo Dunia nzima, huku kiwilaya ya Handeni, yakifanyika katika Kata ya Kwasunga, wilayani Handeni.
Kamanda wa Polisi wa Wilaya Handeni, OCD Zuberi Chembera, wa pili kulia mwenye koti jeusi akionyesha ujuzi wa kusakata rhumba katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, ambapo kiwilaya, yalifanyika Kata ya Kwasunga, ambapoi alimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alihudhuria majukumu mengine ya Kitaifa. 
 Kaimu Mkurugenzi wa Handeni, Mr Mdoe, aliyesimama, akizungumza jambo katika madhimisho ya Ukimwi katika Kata ta Kwasunga, wilayani Handeni mkoani Tanga.
 Kamanda wa Polisi wa Handeni, OCD Zuberi Chembera, akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi duniani, ambapo kiwilaya yalifanyika katika Kata ya Kwasunga wilayani Handeni mkoani Tanga. Chembera alimuwakilisha DC Muhingo Rweyemamu.


Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi wa Wilaya Handeni, OCD Zuberi Chembera, akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wilayani hapa.

Akizungumza mbele ya wananchi waliohudhuria katika maadhimisho hayo, OCD Chembera, alisema wanaume wengi hawapendi kupima afya zao, hususan kujua kama wameambukizwa ugonjwa wa Ukimwi, badala yake wanasubiri matokeo ya wake zao.


 Wanafunzi katika shule ya Sekondari Kwasunga, wakiigiza mbele ya wahudhuriaji katika Maadhimisho ya Ukimwi duniani, katika Kata yao.
 Hapa wanafunzi wakiingia kwa ajili ya kuimba kwaya katika maadhimisho hayo. Hakika yalipendeza kupita kiasi.


OCD Chembera, hapa aliacha kiti na kuwasogelea kwa karibu wananchi kwa ajili ya kuzungumza nao juu ya ugonjwa Ukiwi.


Alisema inapotoke wake zao au wapenzi wao wamepata ujauzito, hugoma kabisa kwenda kupima afya zao, jambo linaloweza kukwamisha harakati za mapambano ya ugonjwa wa Ukimwi ndani nan je ya wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.

"Wanaume tuacheni tabia za kuachia akina mama waende wakapimwe afya zao pale wanapopata ujauzito, maana hiyo si njia nzuri badala yake wote tuwe kitu kimoja na kuyapokea matokeo hayo kwa ajili ya kulinda afya zetu.

"Aidha ni wakati wa kila mmoja wetu kushirikiana kwa dhati katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi ambao unaendelea kuangamiza ndugu zetu, japo kiwilaya maambukizi ya Ukimwi yanaonekana kupungua hadi asilimia 2,” alisema.

Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kwasunga, wananchi wengi walihuudhuria sambamba na kujionea burudani kutoka katika bendi ya Azimio pamoja na magizo kutoka kwa wanafunzi kwenye kata hiyo ya Kwasunga.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...