https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, December 06, 2013

Albert Nyaluke Sanga:Wanaofanikiwa hawalali, wako ngangari

Ujumbe wa Mjasiriliamali
Mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu; nilijichimbia wilayani Mvomero-Morogoro kujifunza na kuangalia fursa ya uanzishaji na uendelezaji wa mashamba ya mifugo (lanchi). Baada ya kumaliza kilichonipeleka, nikiwa na rafiki yangu mjasiriamali anaepambana kwa spidi ya ajabu; George Kisawani, tulipata wasaa wa kumtembelea mama mmoja aitwaye Veronica Urio mkulima aliyefanikiwa sana katika kilimo cha mpunga, anaeishi maeneo ya Dakawa. 
Albert Nyaluke Sanga kulia, akiwa na mjasiriamali Veronika Urio.

Mama huyu alinigusa mno, kwani amekuwa ni mkulima namba moja aliyepewa tuzo ya US AID kupitia mradi wa Feed the Future; kutokana na kufanikiwa kulima kilimo cha kisasa . Kwa mafanikio yake alilikuna hadi baraza la senete la Marekani kiasi ambacho mwaka 2011, walitumwa maseneta wawili kuja katika mashamba ya mama huyu kushuhudia na kujifunza namna anavyofanikiwa katika kilimo hiki cha mpunga ambapo huvuna maelfu ya magunia kila msimu. Kwa kilimo hiki mama huyu anamiliki vitega uchumi vingi kiasi kwamba amepata uthubutu wa kusomesha watoto wake watatu katika nchi za Marekani, Ujerumani na Poland. 


Kilichonikosha ni kuwa mama huyu kielimu ni darasa la saba tu lakini amekuwa ni mtu anaependa kujifunza, kudadisi na kutafuta taarifa sana. Kutokana na faida anayovuna kutoka katika kilimo hicho, amejiwekea utaratibu wa kufanya safari za mapumziko katika nchi za Ulaya na Asia kila mwisho wa msimu wa kilimo. Katika mazungumzo yetu mama huyu alitueleza hivi: 

"Nina jumba la kifahari na kitanda kizuri sana, lakini sikumbatii kitanda kupitiliza. Kila siku ninaamka saa kumi na moja alfajiri na ninarudi nyumbani usiku. Kila mara popote nilipo ninaumiza kichwa ni namna gani nitaendelea kuongeza uzalishaji" Mwisho akatupa wosia, 

"Ikiwa mimi mama yenu na umri huu bado ninajituma kupambana, je, ninyi vijana kwa nini mzembee wakati mna nguvu na uwezo kunishinda? Kuweni ngangari, msilale, changamkeni kuandaa maisha mkingali vijana kwa sababu fursa za kuwa mabilionea zipo katika FIKRA ZENU" ~SmartMind~

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...