https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, December 28, 2013

Vijana waaswa kujituma uwanjani ili wafikie malengo yao

Na Kambi Mbwana, Aliyekuwa Handeni

VIJANA wenye vipaji na uhitaji wa kucheza soka wametakiwa wacheze soka kwa kujituma ili wafikie malengo, badala ya kutegea katika mazoezi hivyo kujiweka katika hatari ya kushindwa kufika mbali na kutimiza malengo yao.


Hayo yamesemwa na kocha wa timu ya soka ya Komsala, wilayani Handeni, mkoani Tanga, Sufian Omary, katika mazoezi ya vijana wake wanaoendelea katika mashindano ya Mbuzi Cup inayokutanisha timu mbalimbali za Kata ya Kwamatuku.


Akizungumza mapema wiki hii wilayani humo, Omary alisema kwamba vijana wengi wanaopenda kuwika katika soka, wameshindwa kufika mbali kutokana na kutegea katika mazoezi yao uwanjani.


“Wachezaji wote wenye malengo yao lazima wafanye mazoezi makali na kuweka bidii uwanjani, hivyo lazima mcheze kwa bidii, ukizingatia kuwa hakuna mashindano madogo hata kama tungekuwa tunagombea kuku.


“Naamini tukifanya hivyo itakuwa ni njia ya kuiweka timu yetu katika nafasi nzuri zaidi, huku ikiwa njia ya wachezaji wenyewe kuwa katika wakati wa kuwaza maendeleo katika mashindano,” alisema.


Timu ya Komsala ni miongoni mwa maeneo yenye wachezaji wazuri kiasi cha kutia hamu kuwaangalia wanavyokuwa uwanjani, huku wakishiriki katika mashindano ya kugombania mbuzi katika Kata ya Kwamatuku, yanayofanyika katika Uwanja wa Kijiji cha Kweingoma.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...