https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, December 22, 2013

Asha Baraka ambana Mbizo sakata la Gurumo


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

MWENYEKITI wa Kamati ya Gurumo (55) Asha Baraka, amembana mratibu wa tamasha hilo Juma Mbizo kwa kumtaka ampelekee ripoti ya matukio yalivyoandaliwa na kufanyika katika onyesho la kumuaga Muhdin Gurumo, lililofanyika Jumamosi ya Desemba 14 mwaka huu.

Mwenyekiti wa iliyokuwa Kamati ya Gurumo, Asha Baraka kulia, katika matukio ya kufanikisha tamasha la mzee Gurumo.

Asha aliyasema hayo huku kukiwa na habari mbaya kutoka kwa baadhi ya wadau waliolalamikia maandalizi pamoja na mgawo wa fedha kwa wale walioalikwa, ukiachwa walioamua kujitolea.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Asha alisema kwamba wakati tamasha hilo la kumuaga Gurumo linafanyika alikuwa nje ya nchi, hivyo amemtaka Mbizo kama mratibu apelike ripoti.


Alisema mara baada ya kuipata ripoti hiyo, kila kitu kitakuwa wazi kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sawa na kulinda heshima kwa wadau wa muziki, wakiwamo wale wanaolalamikia mchakato huo.


Kwa sasa siwezi kusema lolote kwasababu sijapata ripoti ingawa tayari nimeshazungumza na mratibu, Juma Mbizo nikimuomba ailete kwa ajili ya kuangalia jinsi shoo ilivyofanyika,” alisema Asha.


Tamasha hilo liliandaliwa kwa ushirikiano mkubwa wa wadau wa muziki, akiwamo Asha kama mwenyekiti, Said Mdoe, Mbizo na wengineo kwa ajili ya kumuaga Gurumo kutokana na kuachana na muziki.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...