https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, December 29, 2013

Mwimbaji wa Injili Rose Muhando awakuna wakazi wa Tanga


Mwimbaji mahiri wa nyimbo za kiroho a.k.a Injili,na anaetamba na wimbo mpya wa Facebook,Rose Muhando akiwa sambamba na skwadi lake zima wakilishambulia jukwaa vilivyo jioni ya leo ndani ya uwanja wa Mkwakwani wakati wa muendelezo wa tamasha la Krisimasi lililofanyika leo Mkoani Tanga.Tamasha hilo ndio kwa mara ya kwanza linafanyika mkoani humo,limezindundiliwa jijini Dar siku ya Krisimasi ndani ya uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na watazamaji lukuki.Tamasha hilo baada ya kufanyika mkoani Tanga,kesho litafanyika jijini Arusha na baadae mkoani Dodoma likiwajumuisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za Injili.

 Pichani kulia ni Mwimbaji wa kimataifa wa nyimbo za kusifu na kuabudu kutoka nchini Zambia, Epfrahim Sekeleti akiimba pamoja na mwimbaji mwingine mahiri wa nyimbo injili hapa nchini,Bon Mwaitege pichani shoto.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...