https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, July 27, 2014

Yusuf Manji avunja Kamati ya Utendaji, aunda mpya, Ridhiwan Kikwete awekwa kando



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

MWENYEKITI wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji, amevunja Kamati ya Utendaji kuanzia Julai 31 na kuunda mpya kwa ajili ya kusimamia na kuiendeleza klabu hiyo yenye maskani yake jijini Dar es Salaam.
Yusuf Manji, pichani.
Mbali na kuvunjwa kwa Kamati ya Utendaji, pia Manji ametangaza kuzivunja Kamati zote, ikiwamo ile ya kusimamia Jengo la Mafia, ambalo lilikuwa likisimamiwa na Mwenyekiti wake Ridhiwan Kikwete.
WAJUMBE WAPYA WA Kamati ya Utendaji ya YANGA ni hawa WAfuaTAO:

1.    Bw.Abubakar Rajabu                          -           Mradi wa Jangwani City

2.    Bw.Sam Mapande                              -           Sheria na Utawala Bora


3.    Bw.George Fumbuka                         -           Uundwaji wa Shirika


4.    Bw.Waziri Barnabas                           -           Vibali vya Hatimiliki na Mahusiano

na Wafadhili



5.Bw.Abbas Tarimba                                -           Mipango na Uratibu


6.    Bw.Isaac Chanji na Bw.Seif Ahmed  -           Uendelezaji wa Mchezo


7.    Bw.Musa Katabalo                              -           Mauzo ya Bidhaa


8.    Bw.Mohammed Bhinda                      -           Ustawishaji wa Matawi


9.    Bw.David Ndeketela Sekione             -           Uongezaji wa Wanachama


10.  Bw.Mohammed Nyenge                    -           Utangazaji wa Habari, Taarifa,

Matangazo n.k.
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji iliyoundwa upya watasimamia kimsingi kamati ndogo zifuatazo:


·                     Kamati ya Maadili                               -           Bw.Sam Mapande


·                     Kamati ya Nidhamu                            -           Bw.Sam Mapande


·                     Kamati ya Uchaguzi                           -           Bw. Sam Mapande


·                     Kamati ya Uchumi na  Fedha             -           Bw.George Fumbuka na Bw.Waziri

Barnabas

·                     Kamati ya Mashindano                       -           Bw.Seif Ahmed & Bw.Isaac Chanji


·                     Kamati ya Soka la Vijana na


Wanawake                                          -           Bw.Seif Ahmed &Bw.Isaac Chanji


·               Kamati ya Ufundi                                -           Bw.Seif Ahmed &Bw.Isaac Chanji


5.    Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti wa YANGA wanamategemeo makubwa kuwa waliotajwa hapo juu watahakikisha wana timiza malengo yaliyokusudiwa na YANGA ili“DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO” mpaka hapo itakapoamuliwa kubadilishwa au kutenguliwa vinginevyo.


6.    Mwisho,tunawaomba ushirikiano wa dhati ili kuhakikisha kuwa YANGA inapiga hatua mbele na inafanikiwa katika kufikia malengo na mipango yake ya maendeleo ya muda mfupi na ya muda mrefu kwa manufaa ya Klabu, Timu na wana YANGA popote walipo duniani.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...