https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, July 30, 2014

Fiesta kuanzia Mwanza Agosti 9



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WAKAZI na wananchi wa jijini Mwanza, Tanzania, watapata fursa ya kuwa wa kwanza kushuhudia burudani za tamasha la muziki la Fiesta, litakaloanza Agosti 9, CCM Kirumba, Mwanza.

Kuzinduliwa kwa tamasha hilo, ni harakati za mwendelezo wa ziara za mikoani, ambapo wasanii mbalimbali wenye majina yao hupata nafasi ya kupanda jukwaani kutoa burudani.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio, Ruge Mutahaba, alisema kwamba maandalizi ya mwisho yanafanywa ili kuliweka pazuri tamasha hilo.

“Fiesta ni tamasha kubwa ambalo mashabiki nchini kote wanaliheshimu na kuona ni sehemu muafaka ya kupata burudani kabambe.

“Kwa mwaka huu wadau wa muziki wa jijini Mwanza watakuwa wa kwanza kuangalia maudhui na mikakati kabambe ya kuliweka juu tamasha hili linalotamba Tanzania,” alisema.

Wasanii mbalimbali nchini wanajiandaa kwa tamasha hilo, ambalo mara zote limekuwa eneo muafaka la kuwatangaza wasanii ndani na nje ya jiji la Dar es Salaam.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...