https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, July 06, 2014

DC Kilindi aipongeza Tingisha FC



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

MKUU wa Wilaya ya Kilindi, DC Suleiman Liwowa, ameipongeza timu ya Tingisha FC kwa kuonyesha kiwango kizuri katika mashindano ya Gallawa Cup yaliyofanyika jijini Tanga.
DC wa Wilaya Kilindi, Suleiman Liwowa, pichani.
Katika mashindano hayo, Tingisha FC walifanikiwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuwafunga ndugu zao Korogwe kwa bao 3-1.


 Akizungumza mwishoni mwa wiki, DC Liwowa alisema kwamba vijana wake wa Kilindi wameonyesha kiwango cha aina yake na kusisimua wengi katika mpira wa miguu.


 Alisema kuwa anaamini vijana hao wataendelea kufanya mazoezi ili kulinda viwango vyao na hatimaye kutafuta mafanikio zaidi kwenye soka.


Mashindano ya Gallawa Cup yaliandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, maalumu kwa ajili ya kujenga undugu mkoani humo.


“Timu yetu imefanikiwa kushika nafasi ya tatu, lakini kiwango chake ni kizuri na hakika wilaya yangu imefarijika.



No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...