https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, July 30, 2014

Waimbaji wa nchi tano Afrika Mashariki kuchuana vikali

 Allan Kalinga-CEO for Afro-Euro Management Co. LTD
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAIMBAJI kutoka nchi tano katika Kanda ya Afrika Mashariki hadi kufikia mwisho wa mwaka huu wanatarajiwa kushiriki katika shindano jipya la uimbaji liitwalo Shindano la Waimbaji wa Afrika Mashariki.

Shindano hilo ambalo limeandaliwa na Kampuni ya Afro-Euro Events Management Co. Limited, linatarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam, na kuhusisha wasanii nguli kutoka Uganda, Tanzania, Kenya, Rwanda na Burundi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Afro-Euro Management Co. LTD, Allan Kalinga, ambaye kwa sasa makazi yake yako nchini Uingereza, alisema kwamba wagombea  husika watachuana kuwania tuzo ya heshina ya juu kuvikwa taji la muimbaji bora wa eneo la Afrika Mashariki.

 "Umma wa Afrika Mashariki utahusishwa kuanzia mwanzo wa shindano hili hadi mwisho na hivyo mshindi atakayepatikana atakuwa chaguo la kweli la watu wa Afrika Mashariki, " alisema Kalinga.

MCHAKATO WA UTEUZI
Kalinga aliendelea kusema zaidi kwamba  kila nchi shiriki itafanya uteuzi wake wenyewe kuwatambua wanamuziki wake watano bora ambao watawakilisha katika fainali ya kikanda.

"Kila nchi itakaribisha raia wake kutuma mapendekezo yao kuhusu  mwanamuziki bora kwa kutumia namba ya Ujumbe Mfupi wa Maneno  (SMS)  kupitia shirika la simu litakaloteuliwa kwa kipindi cha muda maalum . Shirika hilo la simu litakaloteuliwa litaingia makubaliano na kampuni ya Afro-Euro Management Co. LTD kuhusu gharama za ujumbe mfupi wa maneno (SMS)  na mpangilio wa kugawana mapato, "alibainisha.
Majina yaliyopendekezwa yatalingana  na wanamuziki watakaoshika nafasi za juu nne watakuwa wawakilishi wa nchi husika katika shindano ka kikanda.
Kwa mujibu wa Kalinga, idadi ya mwisho kwa washiriki kutoka nchi hizo tano itakuwa  25 na hawa ndio wanamuziki watakaoshindana  katika Shindano la Waimbaji wa Afrika Mashariki  Dar es Salaam.

MUUNDO WA SHINDANO
Amebainisha kwamba washiriki 25 waliofuzu fainali watagawanywa katika makundi manne ya waimbaji watano, na kila mwimbaji katika kundi atatakiwa kutoka kutoka nchi tofauti.

"Kundi la kwanza lifanya onesho  Jumamosi ya kwanza baada ya kutangazwa wateule 25 watakaoshiriki fainali. Watawasili nchini siku ya Ijumaa, na kufanya onesho Jumamosi na kuondoka Jumapili. Maonesho yatakuwa juu ya jukwaa na kuoneshwa moja kwa moja kwa njia ya televisheni katika nchi zote tano za Afrika Mashariki na  vituo vya Televisheni vitakavyoteuliwa, " alisema Kalinga.

Baada ya maonesho na kwa siku ya sita zitakazofuata, anasema kwamba umma utaalikwa kupiga kura kupitia SMS kwa kutumia namba maalum katika mitandao itakayoteuliwa kwa ajili ya kuwateua wasanii wao bora kati ya kikundi.

"Kura za kundi la kwanza zitajumlishwa na kuthibitishwa na kampuni huru ya ukaguzi wa hesabu, na kutangazwa wakati wa maonesho ya kundi la pili siku ya Jumamosi. Waimbaji watakaoshika nafasi mbili za juu kutoka kila kundi watafuzu fainali, na hivyo kutupa  jumla ya waimbaji 8 watakaoshiriki fainali, " alibainisha.

 Katika kila wiki wakati kura zikiendelea, vyombo vya habari ambavyo kampuni ya  Afro-Euro Management Co. LTD itashirikiana navyo  katika kila nchi zitangaza upigaji kura kwa njia ya  'SMS' katika nchi husika za Afrika Mashariki ya Afrika ili kupata watu wengi iwezekanavyo kushiriki.

 Aidha, Kalinga, ambaye pia kampuni yake ya Afro-Euro Management Co. LTD ndiyo iliyoratibu shindano la ulimbwende la Miss Afrika in UK lililofanyika katika jiji la Reading nchini Uingereza mwaka 2004 - alisema washiriki nane wa fainali kisha watashindana katika Finali Kubwa (Grand Finale).

FAINALI KUBWA
"Jumamosi ya wiki ya tano, washindi wa kundi la mwisho wataungana na washiriki wengine sita waliofuzu fainali katika kufanya maonyesho yao katika Fainali Kubwa . Umma kutoka nchi shiriki kisha utakuwa na siku sita (Jumapili hadi Ijumaa) za kupiga kura kumchagua mshindi pekee, " Kalinga alisema.

Alibainisha kwamba matokeo yatajumuishwa baada ya upigaji kura kufungwa Ijumaa ya wiki ya sita na kuthibitishwa na kampuni huru ya ukaguzi wa hesabu kabla ya tangazo la mwisho la matokeo Jumamosi wakati wa onesho la mwisho litakalooneshwa moja kwa moja kwa njia ya televisheni, akiongeza kuwa idadi ya kura zilizopigwa kwa kila aliyefuzu fainali itaamua ni nani itatangazwa mshindi, mshindi wa pili na mshindi wa tatu.

TUZO & ADA
Aliongeza kusema kwamba kampuni yake ataamua zawadi kwa mshindi, mshindi wa pili na mshindi wa tatu; Na uimbaji/ada ya uimbani kwa washiriki 25 waliofuzu fainali.

MIPANGO YA BAADAYE
Mkurugenzi Mtendaji huyo alibainisha kwamba sehemu ya faida kutokana na shindano hilo itakwenda kwa taasisi ya hisani itakayochaguliwa katika kila nchi shiriki.

Katika siku zijazo, inatazamiwa kwamba raundi ya mtoano katika makundi manne itafanyika katika nchi shiriki nne tofauti huku Fainali Kubwa ikifanyika katika nchi ya tano.

"Tunapanga kuingiza shindano la pili, yaani Shindano la Waimbaki wa Injili Afrika Mashariki. Tunaona mashindano hili litaendana na Shindano la Waimbaji wa Afrika, ambapo bara la Afrika litagawanywa katika kanda, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika Kaskazini, Afrika ya Kati na Kusini mwa Afrika, "alisema.

Kuweza kumudu  changamoto hii kubwa  katika kuandaa na kuendesha mashindano hayo ya kikanda, Kampuni ya Afro-Euro Management Co. LTD,. Inakusudia kuteua kampuni za wakala kushikilia haki za mashindano katika kanda zao husika.

Washindi na washindi wa pili wa kila kanda ya mashindano watafuzu Fainali Kubwa (Grand Finale) ya Shindano la Waimbaji wa Afrika.

ONESHO LA MOJA KWA MOJA
Aidha, Kalinga amesema kwamba washiriki 10 waliofuzu fainali watachuana katika tamasha litakalooneshwa moja kwa moja katika televisheni litakaloitwa TAMASHA LA AFRIKA MASHARIKI.

"Wasanii kumi kutoka nchi tano za Afrika Mashariki watafanya maonesho katika majiji matano katika wiki tano mfululizo ili kuwapa mashabiki wa muziki fursa ya kuona maonesho ya muziki moja kwa moja kutoka kwa wasanii wakubwa katika Afrika ya Mashariki, "alisema.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...