https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, July 04, 2014

DRFA yaipongeza Simba, Aveva kuchaguliwa kwa kishindo


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), kimeipongeza klabu ya Simba kwa kufanya uchaguzi wa amani na kupata viongozi wake wapya watakaoingoza kwa miaka minne.



Mwenyekiti wa DRFA Almas Kassongo, amema kuwa wana imani na uongozi huo mpya wa Rais Evans Aveva, Makamu wake Geofrey Nyange ‘Kaburu’ na Kamati yake ya utendaji.



“Sisi DRFA tunawapongeza viongozi wapya waliochaguliwa kuiongoza klabu ya Simba kwa kipindi cha miaka minne, katika uchaguzi uliofanyika Juni 29 mwaka huu katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Pilisi, Osterbay.



“Tunaamini kuwa wanachama waliowachagua viongozi hao wana imani nao na wataweza kuiongoza klabu hiyo kufikia mafanikio,” alisema Kassongo.



Alisema DRFA itakuwa tayari kufanya kazi na kushirikiana kwa karibu na uongozi huo katika kipindi chote cha uongozi wao na kuwataka kudumisha amani na utulivu ndani ya klabu hiyo.



Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Colin Fish, Jasmine Sudi, Said Tuli, Idd Kajuna na Ally Sum.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...