https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, July 24, 2014

Kutana na damu changa iliyotangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Nkenge (Chadema)

JOTO la kisiasa nchini kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 limezidi kushika kasi baada ya kijana, Edson Joel, kuonyesha nia ya kuwania Ubunge katika Jimbo la Nkenge, akitaka kujitosa kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 Edson Joel pichani akiwa kwenye moja ya majukumu ya kichama jimboni Nkenge.
Edson Joel mwenye kofia akiwa na timu katika moja ya shughuli za kijamii jimboni Nkenge.

Joel ameweka kambi yake ya wiki tatu jimboni humo akishiriki katika kazi mbalimbali za kijamii kwa ajili ya kuangalia namna ya kuwaingilia jimboni humo na lengo lake la kuwatumikia Watanzania, hususan wa Jimbo la Nkenge kutimia.

Joel aliuhakikishia mtandao wa Handeni Kwetu Blog kuwa anazo sifa na nguvu ya kuwatumikia Watanzania kwa kupitia chama chake cha Chadema. Habari mbalimbali juu ya siasa na wanasiasa Tanzania zitaendelea kukujia live...

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...